Tuesday, December 20, 2011

WAKOREA WAOMBOLEZA

 Kim Jong-Un, mrithi wa utawala wa Korea Kaskazini. Ana miaka 29 sasa.
 Rais wa Korea Kaskazini enzi zake, kushoto akiwa na viongozi mbalimbali

 Wakorea Kaskazini wakilia kwa uchungu







Wednesday, October 12, 2011

WARIOBA AWATAKA WATZ WACHAPE KAZI

JAJI WARIOBA AWAONYA WATANZANIA WAACHE KULALAMIKA
*Asifu juhudi za Serikali kuleta maendeleo
 
WAZIRI MKUU Mstaafu, Mheshimiwa Jaji Joseph Warioba amesifu jitihada zilizofanywa na Serikali katika kuleta maendeleo nchini lakini amewaonya Watanzania waache tabia ya kulalamikia kila jambo na badala yake wafanye kazi.
 
Ametoa kauli hiyo leo mchana (Jumanne, Oktoba 11, 2011) wakati akijibu maswali ya waandishi wa habari mara baada ya kutembelea mabanda ya maonesho yaliyoandaliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara.
 
Amesema kuna mambo mengi ambayo yamefanyika tangu nchi ipate uhuru lakini hakuna anayetambua mchango huo na badala yale kila mmoja amekuwa mwepesi wa kutoa lawama. “Kuna kitu kimoja kinachonipa matatizo nacho ni kuona nchi imekuwa ni ya watu waliokata tamaa… wananchi na viongozi ni watu wa kulalamika tu, sisi sote ni walalamikaji,” alisema mbele ya waandishi hao.
 
“Kwa hali ilivyo, nasema tujihadhari kwa sababu tunaweza kupata matatizo ya kiuchumi kwa sababu ya matatizo ya umeme, bei kubwa ya mafuta na kushuka kwa thamani ya shilingi. Kama shilingi itaendelea kushuka, mfumuko wa bei utakuwa mkubwa na atakayeumia ni mwananchi wa kawaida,” alibainisha.
 
Alisema kazi ya kutafuta uhuru ilikuwa ngumu na kulikuwa na baadhi ya watu walioamini kuwa Tanganyika isingepata uhuru wake kwa sababu kazi ya kumtoa Mwingereza haikuwa rahisi. “Mimi ni mmoja wa watu waliokuwepo uwanjani kushuhudia bendera ya Mwingereza ikishusha na kuona bendera ya Tanganyika ikipandishwa.”
 
“Jeuri tuliyokuwa nayo wakati wa harakati za kutafuta uhuru ilikuwa kubwa… dhamira tuliyokuwa nayo ibaki vilevile, tuwe ni watu wa kuthubutu. Kama tuliweza wakati ule, tukiwa hatuna hatuna teknolojia za kisasa kama sasa, naamini hakuna kitu kinachoweza kuturudisha nyuma,” alisisitiza.
 
Alisema umefika wakati wa wananchi kukaa pamoja na kujadili changamoto zinazolikabili Taifa na kukubali kuwa matatizo siku zote yapo. “Matatizo ni sehemu ya maisha, ukithubutu kuyapatia ufumbuzi unaweza kupata suluhu ya matatizo hayo. Maonesho haya yanatukumbusha jinsi tulivyoweza kuthubutu, yanatukumbusha tulikotoka,” alisisitiza.
 
(mwisho)
 
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 3021
DAR ES SALAAM

Tuesday, October 11, 2011

Kumekucha Miss Utalii Dom






Picha zote na Shabani Mpalule, Dodoma

PERUGINA INVESTMENT , SIDE WAY WAJITOKEZA KUDHAMINI MISS UTALII DODOMA

Fainal za Miss Utalii Mkoa wa Dodoma zimepangwa kufanyika kwenye ukumbi Mpya wa Kisasa wa CLUB LA AZIZI,  ikiwa ni mabadiliko ambayo yamefanywa baada ya Mkoa wa Dodoma kutaka kufanyika kwenye ukumbi kutokana na kuwa bora kwa sasa ikilinganishwa na kumbi zingine za mkoa huo.
katika onyesho hilo ambalo awali lilipangwa kufanyika ukumbi wa new Dodoma hotel,  maandalizi yanaendelea kwenye ukumbi wa New Dodoma Hotel na warembo wote wako katika hali ya ushindani ambapo baadhi ya wadhamini wanazidi kujitokeza kusaidia fainal hizo.
Baadhi ya wadhamini walijitokeza ni PERUGINA INVESTMENT CO. LTD, SIDE WAY LODGE, Warembo  wanaoendelea na mazoezi ni pamoja na Jackline Leshange,Bahati Mwinyi,Martha Simon,Elizabeth Ayoub,Magreth Kapelle, Jazila Maulid, Agnes Stephan, Lucy Charlecy, Khadija Ally, Kija Masanja, Tausi Shaaban,Kibibi Aman, Nyabitage King'ala, Joyce Mwakibinga, Axer Peter, Nelly  Fabian Angelo,Anna Gisbert, Janet John, Julieth Katunzi, Ester George, Mary Wilson, Jenifer Kayanda, Bety Magawa,  na  Jackline John , chini ya jopo la wakufunzi(Walimu), ambao ni Miss Utalii Njombe na Balozi wa Hifadhi ya Taifa  ya Kitulo 2010/2011, Neema Isdory, Miss Utalii Tabora na Balozi wa Utalii wa Ndani, Sweet Maliwa,  Miss Utalii Vyuo Vikuu Kanda ya Kati, Tabia Msuta.
Washindi katika Fainal hizo wataungana na Washindi wa wenzao wa Mikoa ya Singida, Tabora, pamoja na Katavi kuunda Kanda ya Kati iliyopangwa kufanyika mwezi wa kumi na mbili kati ya Mkoa wa Dodoma na Tabora.
Katika Onyesho hilo Mgeni Rasmi anatazamiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma pamoja na Waheshimiwa Wabunge wa Mkoa huo ambao ni Wageni waalikwa, Afisa Utamaduni Mkoa, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini, Mkuu wa jeshi la Polisi Dodoma, pamoja na Maraisi wa Vyuo vya Wanafunzi vilivyopo Dodoma.
Wengine  waliojitokeza kudhamini Fainal hizo  Mpaka sasa ni Pamoja na, Kifimbo FM Radio kwa Upande wa (Matangazo), CLUB LA AZIZI,  Asante Water(Maji ya kunywa Washiriki),Ngoto Feniture, Royal Village, Clouds Fm Radio, TANAPA, Ngorongoro Creater, VETA Hotel, Shabibi Bus Service.
wengine ni Tanzania Daima & Sayari News Paper, Image Masters, Papaa Msofe, Zoizzuu Fashion, Dar City College, Kumekucha Action Mart, Viovena & Co LTD, pamoja na waheshimiwa Wabunge wa Dodoma.
Fainal za Miss Utalii Tanzania 2011/2012 Maanadalizi yake yanaendelea katika mikoa yote ya Tanzania ambapo Fainal za Taifa zimepangwa kufanyika pia Katika Mkoa wa Dodoma.


Thursday, October 6, 2011

UBINAFSI-NIUUNAVYO!!

Ubinafsi tu. Kama ni njaa, si wote inauma? Hivi kwa nini ule peke yako, ina maana huoni matumbo ya wenzako?

Ndugu zangu,

Ubinafsi duniani ulianza tangu zamani. Lakini kwa kadri binadamu anavyopiga hatua kimaendeleo, ubinafsi unazidi kukua. Hata hivyo, hakuna jitihada zozote za kijamii angalau za kuhamasisha na kuongeza uelewa wa wanajamii kuhusu madhara ya mtu kuwa mbinafsi.

Kwa tafsiri yangu, Uvunjifu wa maadili, Vita, Ufisadi na mengine mengi ni matokeo ya huu huu ubinafsi kutamalaki.

Pengo kati ya walionacho na wasionacho linazidi kuongezeka. Wengine wanadai hayo ni matokeo ya mfumo wa ubepari ambao unafuatwa na nchi zetu, baada ya ujamaa kuzikwa bila matanga. Hata hivyo, hata huo ubepari tafsiri yangu ni hiyo hiyo ubinafsi. Ila kuna ubinafsi unaopakwa mafuta.

Nawasilisha.

Friday, September 30, 2011

Tuesday, September 27, 2011

BIMA YA NYWELE ZA KIFUA

Are the stars pulling our legs, or are their body parts at special risk? Here's a look at some of the unlikely anatomical assets celebrities got covered.SASA HII KUFURU SASA